Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sarakwa wilayani Bunda mkoani Mara kuhusu umuhimu wa kutoa taarifa mapema kwenye ofisi za kijiji wakati wanyamapori wakali na waharibifu wanapoharibu mazao.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Sarakwa wakimsikiliza Naibu Waziri waMaliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu wakati wa mkutanao wa hadhara uliofanyika katika eneo la Shule ya ,msingi ya Sarakwa mara baada ya kusikiliza malalamiko yao kuhusu malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akisalimiana na baadhi ya watumishi wa wilaya ya Bunda mkoani Mara mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mkuu wa wilaya kwa ajili ya kikazi ya siku moja.
Mbunge wa jimbo la Bunda vijijini, Boniface Getere akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sarakwa kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu kuzungumzia kuhusu umuhimu wa kutoa taarifa mapema kwenye ofisi za kijiji wakati wanyamapori wakali na waharibifu wanapoharibu mazao yao.
Mwenyekiti wa kijiji cha Sarakwa, Samson Kapeta akizungumza na wananchi wake kabla ya kumkaribisha na Mbunge wa jimbo la Bunda vijijini, Boniface Getere kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho.
……………………
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) iunde timu ya kuchunguza uhalali wa malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi kilichotolewa kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori wakali na waharibifu wa mazao katika maeneo mbalimbali nchini.
Mhe. Kanyasu ametoa agizo hilo mara baada ya kupokea malalamiko na madai kutoka kwa baadhi ya wananchi wa vijiji 4 vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, wilayani Bunda mkoani Mara ambao mazao yao yaliliwa na kuharibiwa na wanyamapori wakali wamekuwa hawalipwi huku wasiostahili ndo wamekuwa wanalipwa .
Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Sarakwa, Mariwanda ,Unyali na Kihomboi vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Bunda mkoani Mara, Mhe. Kanyasu amesema kuwa mara baada ya uchunguzi kukamilika wale watakaobainika kupokea fidia hiyo wale wasiostahili watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kuzirudisha fedha hizo.
‘’Nataka niwambie, wale waliopokea kifuta jasho na kifuta machozi kutoka serikalini wakati hawastahili lazima hizo fedha wazitapike” Amesisitiza Mhe. Kanyasu




