Ni sehemu Maarufu inayojulikana

kwa jina la Kijiji cha Wavuvi eneo la Kurasini wilayani Temeke  ambapo kuna ufukwe mzuri wa bahari ambao

kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu ikiwa ni pamoja na uvuvi,

biashara ndogo ndogo na kutupia taka kutoka majumbani  pamepelekea kuwa kero na kusababisha wakazi wa

Temeke na maeneo ya jirani kukosa eneo la kufurahi.

Kwa kuona umuhimu huo na shauku

ya kuwa na sehemu ya ufukwe Taasisi zisizo za kiserikali ikiwa ni pamoja na

TCCI, Mazingira Plus na Sanamare kwa kushirikiana na asasi nyingine zisizo

za kiserikali kama HUDEFO, ETE, Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mazingira TV,

Ofisi ya Mtaa wa Kurasini, wakazi wa eneo la ufukwe na wadau mbalimbali

wameungana kwa pamoja kufanya usafi katika eneo hilo ili hapo baadaye lianze

kutumika kama sehemu ya watu kufurahi na kupumzika.

 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti

wadau mbalimbali wa mazingira wamefurahishwa na hatua hiyo ya kusafisha eneo

hilo la fukwe na kuwaomba wavuvi, wafanyabiashara na wakazi wa maeneo hayo

kuacha kutupa taka na kusema jukumu la kuweka safi eneo hilo sio lazima Serikali

ila wananchi pia wanaweza na kuhimiza kuwa eneo hilo panatakiwa kuwa na Choo ili

kuepuka magonjwa ya mlipuko kwa kuwa mpaka sasa watu wanaofanya shughuli

mbalimbali wanajisaidia vichakani.

Wakati huo huo ETE walishiriki katika kufanya usafi eneo hilo kwa lengo

la kuweka mazingira safi lakini pia kutumia Dijitali kuyasemea mazingira ambayo

hayawezi kujisemea yenyewe, kwa Hashtag #ETEMazingiraKidijidali kwa kutumia mitandao ya

kijamii na majukwaa mbalimbali ya mtandaoni.