Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Mhe. Charles Kichere alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimtambulisha Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Mhe. Charles Kichere (wa pili kushoto) kwa Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge za Hesabu za Serikali za Mitaa, Mhe. Vedasto Ngombale (Kulia), Kamati ya Hesabu za Serikali, Mhe. Nangenjwa Kaboyoka (wa pili kulia) na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Mhe. Mashimba Ndaki
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiagana na Maafisa waandamizi kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) baada ya kujitambulisha kwake leo Bungeni Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wanne kulia mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa waandamizi kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) walioongozwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Mhe. Charles Kichere (wa nne kushoto mbele) leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)