Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana la
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa Edward Simbey
akizungumza jana na wananchi Kijiji cha Kwebada Kata ya Kwebada
wilayani Muheza wakati Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga (Chadema)
Yosepher Komba
alipokwenda kukabidhi saruji na vifaa vya umeme kwa ajili ya ofisi ya
serikali ya Kijiji hicho ambavyo alihaidi

Sehemu ya Saruji iliyotolewa na Mbunge wa
Viti Maalumu (Chadema) Mkoa wa TangaYosepher Komba

AMbunge wa Viti Maalumu (Chadema) Mkoa wa
TangaYosepher Komba akizungumza wakati wa halfa hiyo kushoto ni
Katibu Mwenezi wa Baraza la
Vijana la Chama
hicho Taifa(Bavicha) Edward Simbey kulia ni
Mwenyekiti wa Kijiji Cha Kwabada Joseph
Emanuel

Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana la Chama
hicho Taifa(Bavicha) Edward
Simbey.akizungumza wakati wa halfa hiyo kulia ni Mbunge wa Viti
Maalumu (Chadema) Mkoa wa Tanga

Yosepher Komba

Normal
0

false
false
false

EN-US
X-NONE
X-NONE

/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:”Table Normal”;
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-qformat:yes;
mso-style-parent:””;
mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;
mso-para-margin-top:0in;
mso-para-margin-right:0in;
mso-para-margin-bottom:10.0pt;
mso-para-margin-left:0in;
line-height:115%;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:11.0pt;
font-family:”Calibri”,”sans-serif”;
mso-ascii-font-family:Calibri;
mso-ascii-theme-font:minor-latin;
mso-hansi-font-family:Calibri;
mso-hansi-theme-font:minor-latin;}

AKatibu Mwenezi

wa Baraza la Vijana la Chama

hicho Taifa(Bavicha) Edward Simbey kushoto akikabidhi mpira kwa ajili

ya vijana kushiriki kwenye michezo kwenye Kata hiyo kushoto

anayeshuhudia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (Chadema) Yosepher
Komba

MBUNGE wa Viti

Maalumu Mkoa wa Tanga (Chadema) Yosepher Komba akichukua kero za wananchi
kwenye Kata ya Kwabada wilayani Muheza

Sehemu ya

viongozi wa Chadema na wananchi wa Kata ya Kwabada wakimsikiliza

Mbunge huyo

MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga kupitia Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) Yosepher Komba amekabidhi vifaa vya umeme na mifuko 30 ya
Saruji kwa ajili ya kuchangia miradi ya maendeleo kwenye Kata ya Kwabada
wilayani Muheza.

Halfa ya makabidhiano hayo ilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye Kata
hiyo  na kuhudhuriwa na viongozi
mbalimbali wa chama hicho akiwemo Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana la Chama
hicho Taifa(Bavicha) Edward Simbey.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo Katibu huyo aliwataka
viongozi wa kisiasa kutokubagua wakati wakichangia maendeleo ya wananchi
kutokana na itikadi za vyama kwani hali hiyo inaweza kuwarudisha nyuma

Alisema kuwa viongozi wa kisiasa wanajukumu la kuhakikisha wanawatumikia
wananchi wao bila ya kuweka ubaguzi wa itikadi za vyama kwani kwa kufanya hivyo
wanasababisha kuzorotesha maendeleo .

Akitoleo mfano mbunge huyo ambaye ni wa kuteuliwa kupitia chama hicho lakini
ameweza kutoa msaada huo kwa ajili ya uwekaji wa umeme katika ofisi ya Mtendaji
na saruji kwa ajili ya ujenzi wa darasa bila kujali itikadi za kisiasa kwa
sababu anajua huduma zitakazotolewa zitawagusa wananchi wa vyama vyote.

Katibu huyo pia aliwataka wananchi hao kuhakikisha wanashirikiana bila
kuweka ubaguzi katika utekelezaji wa miradi ambayo inagusa maslahi ya jamii
yote ili kuharakishia huduma na maendeleo yao.

Akieleza namna alivyobaini changamoto hiyo na kuweza kuipatia ufumbuzi
Mbunge wa viti maalum CHADEMA Yosepher Komba alisema kuwa wakati wa ziara yake
ya kutekeleza majukumu ya ubunge Jimboni hamo aliweza kupita katika kata hiyo
na kukutana na changamoto ya ukosefu wa umeme katika ofisi ya Kijiji pamoja na
uhaba wa vyumba vya madarasa.

Kutokana na kuwepo kwa changamoto hiyo niliwahaidi kwamba nitapeleka vifaa
vya umeme kwa ajili ya kuweka katika ofisi ili huduma ya umeme iweze kupatikana
na wananchi waweze kupata huduma bila yavikwazo vyovyote.

Hata hivyo alisema kwamba msaada huo wa Saruji utawasaidia kuweka kufanya
umaliziaji katika ofisi hiyo lakini huku akisisitiza pia umuhimu wa kumalizia
chumba cha darasa ili watoto wetu waweze kusoma bila kuwepo kwa vikwazo vya
namna yoyote ile.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji Cha Kwabada Joseph Emanuel alisema
kuwa msaada huo itasaidia ofisi hiyo kuwa na huduma ya umeme pamoja na
ukamilishaji wa darasa katika shule ya msingi Kwabada.