
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango leo tarehe 6 Juni 2022 akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam aliporejea nchini akitokea Stockholm nchini Sweden alipohudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Stockholm +50.


